Tuesday, September 9, 2014


Worth more? Paul Pogba (right) will earn just £23,000-per-week from his current deal with Juventus
Anataka zaidi? Paul Pogba (kulia) atalipwa paundi elfu 23 kwa wiki kwa wakati huu katika klabu yake ya Juventus

LIGI ya Italia imeshuka umaarufu wake ukilinganisha na ligi nyingine za ulaya na hii inatokana na mishara ya wachezaji wa Seria A iliyotangazwa jumatatu ya wiki hii.
Daniele de Rossi  ndiye mchezaji anayelipwa zaidi ambapo anachukua paundi laki moja kwa wiki na Gonzalo Higuain anamfuatia kwa kulamba paundi elfu 84 kwa wiki na wa tatu ni Carlos Tevez anayepokea paundi elfu 70 kwa wiki. 
Kwa mujibu wa gazeti la Gazzetta dello Sport, klabu za Serie A kwa sasa zinatumia karibia paundi milioni 500 kwa ajili ya malipo ya mishahara wa wachezaji chini ya kiwango cha mwaka 2011 na wachezaji wanaolipwa zaidi wanachukua hela ndogo ukilinganisha na wachezaji nyota wa ligi kuu England na La Liga.
Kwa mfano, Paul Pogba, anapokea paundi elfu 23 kwa wiki msimu huu licha ya kuwa miongoni mwa vijana wenye kiwango cha juu duniani na katika klabu yake ya Juventus.
Juventus, ndio klabu inayoongoza kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya mishara na ni klabu pekee ya Italia ambayo inaongeza mishahara ya wachezaji kutoka 2013/2014 ambapo Carlos Tevez na Arturo Vidal sasa wanapokea zaidi ya paundi elfu 60 kwa wiki.
Nyota wa Roma, Daniele De Rossi ndiye analamba mkwanja mrefu katika mkataba wake wenye thamani ya paundi milioni 5.2 bila kujumuisha posho.
Nyota wa zamani wa Cheslea na sasa Roma  Ashley Cole aliamua kwenda Italia baada ya kutoongezewa mkataba Chelsea na amesaini mkataba atakaomfanya apokee paundi elfu 35 kwa wiki katika kikosi hicho cha Rudi Garcia.
Big money: Former Manchester City striker Carlos Tevez (left) is the top earner at Juventus
Pesa ndefu: Nyota wa zamani wa Manchester City, Carlos Tevez (kushoto) ndiye analipwa zaidi katika klabu ya  Juventus
Love of the game: Ashley Cole (right) has taken a wag cut to join Roma and will earn £35,000-per-week
Mpenda soka: Ashley Cole (kulia) aljiunga na Roma na analamba paundi elfu 35 kwa wiki 

ROMA - Wanaolipwa zaidi

1. Daniele de Rossi - Paundi 100,000-kwa wiki
2. Marco Borriello - Paundi 54,000-kwa wiki
3. Miralem Pjanic - Paundi 49,000-kwa wiki
4. Gervinho - Paundi 45,000-kwa wiki
5. Kevin Strootman - Paundi 43,000-kwa wiki
 
8. Ashley Cole - Paundi 35,000-kwa wiki   

JUVENTUS - Wanaolipwa zaidi

1. Carlos Tevez - Paundi 69,000-per-kwa wiki
2. Gianluigi Buffon - Paundi 61,000-kwa wiki
3. Arturo Vidal - Paundi 61,000-kwa wiki
4. Andrea Pirlo - Paundi 58,000-kwa wiki
5. Fernando Llorente - Paundi 54,000-kwa wiki 
 
15. Paul Pogba - Paundi 23,000-kwa wiki 

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog