Tuesday, September 23, 2014


Aliyekuwa Rais wa TFF, Leodigar Chila Tenga alikuwa mchezaji muhimu wa Taifa Stars miaka ya 1980
HISTORIA inaonesha kuwa zamani mpira wa miguu ulikuwa unachezwa kutoka ngazi ya chini mpaka juu na walipatikana wachezaji wengi wa kulisaidia taifa.
Taifa Stars iliyoshiriki michuano ya mataifa ya Afrika nchini Nigeria miaka ya 1980, ni ushahidi tosha juu ya suala hilo.
Katika kipindi hicho kisichosahaulika miongoni mwa wadau wengi wa soka nchini, wachezaji waliounda Taifa  Stars walitoka timu mbalimbali za chini na za juu. Klabu kubwa za Simba na Yanga hazikutoa wachezaji wake kwa asilimia kubwa.
Leo hii klabu moja inakuwa na wachezaji 6, 8 mpaka 10 katika kikosi cha Taifa Stars. Zamani haikuwa hivi, Simba na Yanga miaka ya 80 wakati Stars ikiifunga Kenya, Harambee Stars 5-0 zilitoa wachezaji wanne tu (kila timu wawili).
Hii ilitokana na kuwepo wachezaji wengi sana. Makocha wa Stars walikuwa na wigo mpana wa kuteua wachezaji kutoka klabu mbalimbali hadi za daraja la pili. Mashindano yalikuwa mengi mno kuanzia chini na mpira ulipigwa kila kona ya nchi.
Leo hii mambo ni tofauti kabisa, mpira hauchezwi kwa misingi mizuri. Hakuna mashindano  mengi maalumu. Taifa Stars inategemea wachezaji kutoka Yanga, Simba na Azam fc.
Kutokana na mazingira hayo, wachezaji wamebaki walewale kila siku. Leo hii kocha wa Stars, Mart Nooij akimuacha Mrisho Ngassa, unadhani ni mchezaji gani mwenye kiwango cha juu atabadili nafasi yake?
Nani anaweza kurithi vizuri nafasi ya Kelvin Yondani, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Mbwana Samatta au Thomas Ulimwengu? Makocha wamejikuta hawana machaguo kwasababu ndio wachezaji waliopo katika kiwango cha juu kwasasa.
Taifa Stars enzi hizo ilikuwa moto wa kuotea mbali

Kocha amekosa wigo mpana wa kuchagua wachezaji wa Stars, lakini zamani kocha alikuwa anaamua mwenyewe amchukue mchezaji wa aina gani na haikuwa lazima kuzifikiria Simba na Yanga .
Ukweli ni kwamba wachezaji wengi ambao waliibuka na kuwa  nyota wa Tanzania walitoka ligi za mchangani.
Ligi hizi zilikuwa na ushindani na hamasa kubwa, kwahiyo Dr Mwaka Sports Xtra Ndondo Cup inajaribu kurudisha hali hiyo na kutoa fursa kwa vipaji vingi vilivyopo mtaani na kuvipatia jukwaa la kuonekana.
Haya sio mawazo mpya, tayari yalishafanyika huko nyuma, lakini michuano hii inakuja kwa ‘staili’ nyingine ya kileo na itatangazwa.
Wachezaji bora wa mashindano watapatikana na kutafutiwa njia ya kuweza kuwaendeleza.
Pia lengo ni kuzitengenezea klabu kubwa sehemu ya kutafuta wachezaji wapya kuliko kusajili hovyo hovyo. Kwasasa hakuna wigo mpana wa kusajili wachezaji, hivyo michuano hii inataka kuibua vipaji vingi vilivyopo mitaani.
Kwa mfano Mtibwa Sugar kila mwaka inauza wachezaji, lakini bado inaendelea kuwepo na kutafuta vipaji vipya kutoka mchangani. Wachezaji wapo wengi, lakini hakuna mashindano.
Kutokana na mazingira haya, Sports Xtra ya Clouds fm imeamua kuanzisha mashindano yanayokwenda kwa jina la DR MWAKA SPORTS XTRA NDONDO CUP.
Banner Ads Top
Michuano hii itakayoendeshwa kwa mfumo wa kisasa kabisa itashirikisha wachezaji wa mchangani kutoka timu 32.
Kivumbi kinatarajia kuanza  Septemba 27 mwaka huu ambapo mechi ya ufunguzi itawakutanisha  Friend’s Rangers na Kiluvya United katika uwanja wa Makulumla, Magomeni, Dar es salaam, majira ya saa 10:00 jioni.
Mbali na dimba la Makulumla, viwanja vingine vitakavyotumika katika mashindano hayo ni Kinesi (Shekilango), Benjamini Mkapa (Ilala) na Mizinga (Kigamboni).
Timu 32 zitakazoshiriki zimepangwa katika makundi nane yenye timu nne.
Kundi A: Boom fc, Beira Hotspurs, Tabata fc na Tuamoyo
Kund B: Sifa Politani, Vijana Ilala, Kijichi, Micco Villa
Kundi C: Friend’s Rangers, Temeke Market, Kiluvya United na Muheza fc
Kundi D: Ukonga United, Sinza Stars, Congo Shooting na Snow White
Kundi E: Zakhem, Black Six, TP Same na Makumba
Kundi F: Villa Squad, Scud fc, Nyota Afrika na Burudani fc
Kundi H: Stakishari fc, Abajalo, Shelaton na Kimara United

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog