Sunday, August 10, 2014


PBP_4315
baadhi ya wadau wa Bavaria wakibadilishana mawazo wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na jovet Tanzania limited wasambazaji wa kinywaji cha Bavaria eneo la afrika mashariki
PBP_4328
Ndugu Justus kyolike meneja masoko mkazi wa Bavaria akiteta na wadau wa Bavaria
PBP_4484
Mkurugenzi mkuu wa Jovet Tanzania Limited ndugu John Kessy akitafakari jambo wakati wa chakula cha jioni alichowaandalia wakala wa Bavaria eneo la afrika ya mashariki.
PBP_4677
Ndugu John Kessy mkurugenzi wa kampuni ya Bavaria akimpongeza innocent gasangwa, wakala wa Bavaria kutoka nchini Rwanda
………………………………………………………………………………………………………………..
Wakati uchumi wa Tanzania ukiendelea kukua siku hadi siku, ongezeko la wananchi wenye kipato cha kati nalo limezidi kukua, na hivyo kuleta changamoto mpya katika masoko ya bidhaa mbalimbali hapa nchini.
Waagizaji wa kinywaji Kutoka Uholanzi cha Bavaria eneo la Afrika ya Mashariki, Jovet (Tanzania) Limited wamedhamiria kuleta changamoto hiyo baada ya kuzindua kampeni rasmi ya mbio za kuelekea kileleni, na hivyo kuongeza wigo wake katika soko hili la Afrika ya Mashariki, ambalo limekua likikua kwa kasi kiuchumi.
Akiongea katika chakula cha jioni na mawakala wakubwa wa kinywaji hicho katika eneo la Afrika ya Mashariki katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam, bwana John Kessy, Mkurugenzi mkuu wa Jovet (Tanzania) Limited, alisema, Kampeni hii ya Bavaria ya kuelekea kileleni imelenga kuleta changamoto kubwa katika eneo hili la Afrika ya mashariki, kwa kuwa litasaidia kutengeneza ajira zaidi, na kuongeza kipato binafsi na kwa serikali kwa ujumla. Bwana Kessy aliongeza na kusema kuwa, Tumeweza kupenya katika soko hili na kutengeneza mahusiano mazuri na wafanyabiashara. Tutaendelea kukua siku hadi siku tukiwapatia wateja wetu kilicho bora zaidi.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia hamsini ya wanywaji wa vinywaji vya shayiri wako eneo la Mashariki ya kati na Afrika na asilimia hii hutumia hektolita milioni 18 kwa mwaka, na hii imetokana na kwamba watu wengi wamekua wakijali zaidi afya zao, na hivyo Bavaria inataka kutumia fursa hii kujikita zaidi katika eneo hili, na kuwapa fursa walaji kupata uchaguzi zaidi.
Mawakala hawa pia waliweza kupata fursa ya kujifunza mengi kuhusu kinywaji cha Bavaria, na pia mbinu za kufanya biashara katika siko hili ambalo limekua likikua kwa kasi na lenye ushindani mkubwa. Pamoja na kujifunza mengi kuhusu Bavaria na mbinu za kibiashara, mawakala hao pia waliweza kujishindia zawadi mbalimbali, zikiwemo seti za Televisheni, Simu za Mkononi na vinywaji mbalimbali vya familia ya Bavaria.
Takwimu za hivi karibuni za mwaka 2010-2015 zinaonyesha kuwa soko la vinywaji linatarajiwa kukua na kuzalisha zaidi ya dola za kimarekani bilioni 1.9, na tafiti hii imefanywa na kampuni ya MarketLine.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog