Thursday, July 10, 2014


Head coach Louis van Gaal of the Netherlands looks on prior to the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.
KOCHA wa Netherlands Louis van Gaal ametoboa kuwa alipata shida sana kumpata Mchezaji wa kupiga Penati ya Kwanza ilipofikia hatua ya Mikwaju ya Penati Tano Tano baada Timu yake na Argentina kutoka 0-0 katika Dakika 120 za Nusu Fainali ya Kombe la Dunia hapo Jana.
Kwenye Penati hizo, Argentina waliibuka kidedea kwa kushinda Penati 4-2 baada Holland kukosa Penati mbili zilizopigwa na Ron Vlaar na Wesley Sneijder na Kipa Sergio Romero kuokoa.
Beki Ron Vlaara ndie aliepiga Penati ya Kwanza.
Lakini Louis van Gaal, ambae Timu yake iliitoa kwenye Robo Fainali Costa Rica kwa Penati ambazo mbili kati yake ziliokolewa na Kipa wa Akiba Tim Krul alieingizwa Dakika za Mwishoni kwa ajili tu ya Penati, Jana alishindwa kutumia mbinu hiyo hiyo baada ya kuwa tayari washabadilisha Wachezaji Watatu.
Head coach Louis van Gaal of the Netherlands instructs to Daryl Janmaat before the extra time during the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.Akiongea na Wanahabari mara baada ya Mechi, Van Gaal alisema: “Ile na Costa Rica ingetupa imani kwani tulipiga vizuri sana. Lakini tatizo lilikuwa nani apige ya kwanza na niliwaomba Wachezaji Wawili na mwishoe nikaangukia kwa Vlaar. Yeye ndie alikuwa Mchezaji bora hivyo angekuwa anajiamini mno. Lakini hii inaonyesha jinsi ilivyokuwa ngumu kupiga Penati kwenye Penati Tano Tano.”
Aliongeza: “Ni mbaya mno, kupoteza Mechi kwa Penati. Ukiondoa yote, tulikuwa sawa na wao, kama sio Timu bora. Inahuzunisha sana!”

Lionel Messi of Argentina shoots and scores a goal in a penalty shootout during the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between the Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.Messi akifunga penati
 Kwenye Mikwaju Mitano ya Penati, Lionel Messi alianza kuifungia Argentina na Ron Vlaar kukosa kwa Netherland baada Kipa kuokoa, kisha Arjen Robben akafunga na Ezequiel Garay kuipa Argentina 2-1.
Sergio Romero of Argentina reacts after saving the penalty kick of Wesley Sneijder (not pictured) in a shootout during the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between the Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.Sergio Romeo akiokoa mkwajuWesley Sneijder alikosa penati...!
Maxi Rodriguez of Argentina shoots and scores his penalty kick in a shootout to defeat the Netherlands during the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between the Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.Maxi alifunga penati..
Akaja Wesley Sneijder na kukosa kwa Kipa kuokoa huku Sergio Aguero akifunga na Argentina kuwa 3-1 mbele.
Dirk Kuyt akafunga kwa Netherlands na kuwa 3-2 lakini Maxi Rodriguez akapiga Penati ya 4 na Argentuna kushinda 4-2.
Maxi Rodriguez of Argentina celebrates after scoring a penalty in the penalty shootout to win the 2014 FIFA World Cup Brazil Semi Final match between Netherlands and Argentina at Arena de Sao Paulo on July 9, 2014 in Sao Paulo, Brazil.Maxi akishangilia penati aliyofungaFuraha kwa Wachezaji wa Argentina baada ya kufunga mikwaju ya penatiKipa wa Netherlands hoi!!!

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog