Monday, July 21, 2014


Legend: Mourinho (left) brought Drogba to the club in 2004 from Marseille, and his faith paid off
Gwiji: Mourinho (kushoto) alimleta Drogba Chelsea mwaka 2004 kutokea klabu ya Marseille.

Imechapishwa Julai 21, 2014, saa 6:35 mchana

NDOTO ya Didier Drogba kurudi tena Chelsea inatarajia kukamilika wiki hii.
Mazungumzo ya kumpa mkataba wa mwaka mmoja wa ukocha na mshambuliaji wa akiba yamekuwa yakiendelea vizuri na kuelekea kukamilika na gwiji huyo wa darajani mwenye miaka 36 ataungana na kocha wake wa zamani, Jose Mourinho.
Inafahamika kuwa Drogba ameshawatumia ujumbe baadhi ya wachezaji wenzake wa zamani wa Chelsea akieleza kuwa anarudi darajani.
Elsewhere: The 36-year-old has interest from clubs in Qatar while Juventus continue to flirt with the idea
Nyota huyo mwenye miaka 36 amezivutia klabu kadhaa nchni Qatar, wakati Juventus wakipambana namna ya kuinasa saini yake.

Chelsea inataka kupunguza wachezaji wenye umri mkubwa kwenye kikosi chake, lakini inatambua mchango wa Drogba nje na ndani ya uwanjani.
Wanaamini kuwa uzoefu wa mshambuliaji huyo utakuwa na ushawishi mkubwa katika benchi la ufundi na atatoa msaada kwa nyota mpya, Diego Costa.
Chelsea wametumia vizuri majira haya ya kiangazi na wataendelea kuongeza wachezaji, lakini wamempoteza Samuel Eto`o na Demba Ba, wakati Romelu lukaku anaweza kujiunga na  Everton licha ya awali kuwepo kwa mipango ya kumrudisha.
Kuwa kocha mchezaji kutasaidia kwenda na sheria ya matumizi ya fedha kwasababu mshahara wake utaingia kwenye bajeti ya makocha.
Drogba alisaini kwa mara ya kwanza Chelsea miaka 10 iliyopita na kuondoka mwaka 2012.
Kuthibitisha kuondoka kwake, Drogba aliiambia tovuti ya klabu kuwa: "Nataka kumaliza tetesi zote na kuthibitisha kwamba naondoka Chelsea. Yamekuwa maamuzi magumu kwangu kufanya na ninajivunia kwa kile tulichopata".
"Lakini muda wa changamoto mpya kwangu umefika. Kama sehemu ya timu nimesaidia sana na kushinda kila kombe lililowezekana".
Milking the applause: Drogba shows his appeciation to the fans during his last game at Stamford Bridge in blue
Drogba alipokuwa akiwashukuru mashabiki wa Chelsea katika mchezo wake wa mwisho ndani ya dimba la  Stamford Bridge. 

KUFURU REAL MADRID!, DILI LA JAMES RODRIGUEZ KUTUA BERNABEU WIKI HII LAKAMILIKA!

Deal me in: Colombia World Cup ace James Rodriguez is set to sign for Real Madrid on Wednesday+9
Anatua Bernabeu: Mchezaji wa Colombia aliyeng`ara kombe la dunia na kutwaa tuzo ya mfungaji bora, James Rodriguez anatarajia kujiunga na Real Madrid jumatano.

Imechapishwa Julai 21, 2014, saa 5:56 asubuhi

NYOTA wa kombe la dunia, James Rodriguez, jumatano ya wiki hii atasaini mkataba na Real Madrid utakaogharimu ada ya uhamisho ya paundi milioni 60.
Rodriguez alikuwa nchini Hispania jana jumapili akitokea kwao Colombia na anaelekea katika klabu ya Manaco ambapo ataaga wiki hii kabla ya kurudi tena mjini Madrid kusaini mkataba wa miaka sita.
Rais wa Real Madrid , Florentino Perez yuko Marekani kusini kwa masuala ya kibishara, lakini anarejea wiki hii kuhakikisha kuwa mabingwa hao wa Ulaya wanatumia zaidi ya paundi milioni 80 kwa kumuongeza Rodriguez baada ya kumsajili Toni Kroos kutoka Bayern Munich wiki iliyopita kwa dau la paundi miliobi 20. 
Golden boy: Rodriguez is due to sign a six-year contract with the La Liga giants this week
Kijana wa dhahabu: Rodriguez anatarajia kusaini mkataba wa miaka sita wiki hii na miamba ya La Liga.
Keep it up: Real will be hoping the 21-year-old attacking midfielder can replicate his World Cup form
Endelea hivyo hivyo: Real wanaamini nyota huyo mwenye miaka 21 anaweza kuonesha kiwango chake cha kombe la dunia 
Big move: Rodriguez was in Spain on Sunday on his way back from Colombia to Monaco+9
Uhamisho mkubwa: Rodriguez alikuwa Hispania akitokea Colombia na anakwenda Monaco kuaga.

Msimu uliopita, mchezaji Gareth Bale alisajiliwa kwa dau la paundi milioni 85 ambapo Real Madrid walimuuza Mesut Ozil kwenda Asernal kusaidia kupata hela ya kulipa mkwanja huo.
Usajili huu mwingine mkubwa majira haya ya kiangazi, unaweza kusababisha angalau mchezaji mmoja au watatu kuondoka ili kupata hela.
Manchester United wanaiwinda saini ya Angel Di Maria licha ya msimamo wa kocha Carlo Ancelotti kutaka Muargentina huyo abaki klabuni hapo.
Kuvunja benki ili kumnunua Rodriguez kunaweza kuwashawishi zaidi Madrid kumuuza Sami Khedira na kushuka dau walililotaja la paundi milioni 20.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog