Saturday, March 8, 2014


Nightmare: Torres has struggled to make an impact since £50m switch from Liverpool
Klabu ya Inter Milan imetoa ofa ya paundi mil 20 kwa Chelsea ili kumsajili mshambuliaji wake mkongwe Fernando Torres. Milan wamefikia uamuzi huu baada ya maneno ya Mourinho aliyoyatoa wiki mbili zilizopita kuwa anahitaji kusajili mshambuliaji mpya kutokana na ubutu wa washambualiaji alionao. Kutokana na kauli hii ya Mourinho mshambualiji huyu amekuwa hana raha ikizingatiwa kuwa Eto'o ndiye anapewa nafasi zaidi kwenye mechi nyingi kubwa. Uwezekano wa mchezaji huyu kwenda Inter Milan msimu ujao ni mkubwa kutokana na mipango mikubwa ya klabu hii kutaka kujiimarisha na kurudisha jina lake. Inter Milan tayari imeshamsajili Nemanja Vidic na itaendelea kutafuta wachezaji wengine wenye majina.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog