Tuesday, January 7, 2014


Chama cha UKIP kinachopinga swala la uhamiaji kinasemekana kuungwa mkono sana
Zaidi ya robo ya raia wa Uingereza wanataka kuona swala la uhamiaji likikomeshwa.
Hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na BBC.
Takwimu hizi ni za kustaajabisha. Asilimia 77 ya waliohojiwa wanasema wanataka uhamiaji kupunguzwa kiasi, zaidi ya nusu wanasema inafaa kukomeshwa kabisa.
Tangu mwaka 1997 karibu watu milioni 4 waliingia nchini Uingereza na maoni yanazidi kuonesha kuwa swala la uhamiaji ni tata sana Uingereza kuliko mataifa mengine ya muungano wa Bara Ulaya.
Lakini mgawanyiko wa kisiasa ungali ukishuhudiwa katika muungano wa kisiasa kuhusiana na swala hilo.
Katika mahojiano na BBC, Waziri wa chama cha Liberal Democrat anasema kuwa wale Conservatives wametangaza nia ya kupunguza uhamiaji iwe chini ya watu laki moja kwa mwaka haufai na haina maana.
Mhariri wamaswala ya kisiasa wa BBC anasema kuwa swala la uhamiaji limekuwa midomonmi mwa wengi Uingereza hasa uchaguzi mkuu ukitarajiwa mwaka ujao. Wengi wanaonekana kuunga mkono chama cha kisiasa cha UKIP chenye sera yake kuu ya inayopinga uhamiaji.
Chama tawala cha Conservative nacho kimeahidi kupunguza idadi ya wahamiaji nchini Uingereza.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog