Wednesday, December 18, 2013


Mbunge wa Iramba Magharibi, mh. Mwigulu Nchemba  leo  asubuhi  aliomba  mwongozo  wa  Spika  wa  bunge  akimtuhumu Mh. Mbowe  kwamba  amekuwa  akitumia  madaraka  yake  vibaya  kwa  kuchanganya  mapenzi  na  kazi, hali  inayolichafua  bunge  la  Tanzania  katika  tawsira  za  kimataifa.....

Mwigulu  ameliambia  bunge  kuwa ,  Mbowe alipiga  simu  kutaka  kusitishwa   kwa  safari ya
mbunge wa viti maalumu Chadema mkoa wa Arusha Joyce Mukya (inasemekana ni mpenzi wake) aliyekuwa  ametumwa  na bunge   kwenda  Dominica Republic  kwa  ajili  ya  kazi  za  bunge....
 
Kwa  mujibu  wa Mwigulu, Joyce  akiwa  huko  alipigiwa  simu  na  Mbowe  akimtaka  akatishe  safari  hiyo  na   badala yake  aelekee  Dubai  kula bata  na Mbowe, kitu  ambacho  amedai  kuwa  ni  matumizi  mabaya  ya  pesa  za  bunge ( posho) ...

Aidha , Mwigulu ameliomba  bunge  lifanye uchunguzi  kuhusu posho zilizotolewa  kwa mbunge huyo ambaye  alikatisha  safari  halali  ya  bunge  na  kumfuata  mpenzi wake ( Mbowe )  Dubai.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog