Wednesday, December 18, 2013

Mpira ulistishwa kwa muda baada ya kutokea upepo mkali na hali ya hewa mbaya huku mabarafu yakianguka hali iliyomfanya mwamuzi kusimaisha mpira kwa dakika chache kama 10 kwenye uwanja wa Stoke City Britannia Stadium.
Kipindi cha kwanza kilimalizika wakiwa nguvu sawa ya bila kufungana. Ndipo kipindi cha pili United wakafanya mabadiliko Anderson akatoka na nafasi yake ikachukuliwa na Chicharito na mpira ukabadilika kwa upande wa United mashambulizi yakazidi.
Kipindi cha pili dakika ya 62 Ashley Young akaachia shuti kali lililomshida kudaka kipa wa Stoke Thomas Sorensen na kuzama hadi ndani ya nyavu za Stoke City. Bao la pili kwa United limefungwa na Evra dakika ya 78 baada ya kupewa pasi na Young na hatimaye Evra kupaisha kwa juu mpira na kumfunga kipa wa Stoke kiulaini. Manchester leo wamecheza bila nyota wao Wayne Rooney na mastaa wengine!
 
 
Mpira ulilazimika kusimama kama dakika 10, wachezaji wa Stoke City wakitoka uwanjani kwa muda baada ya hali ya hewa kuchafuka..
RATIBA
ROBO FAINALI  

Jumatano Desema 18
Stoke 0 v Man United 2
Tottenham 1 v West Ham 2

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog