Friday, July 12, 2013


Katika umri wa miaka 76 amekuwa jina linatamba na nyota wa kurasa za mbele za majarida.
Lakini Papa Francis kwa sasa anapambana kwa nguvu zote kuepuka kuwa mtu maarufu - ameamuru kuondolewa kwa sanamu yake  kwenye kanisa kuu la mjini Buenos Aires.
Tangu kusimikwa kwake waumini wamekuwa wakitembelea sanamu hiyo iliyoko katika bustani ya kanisa kutoa heshima kuu kwa baba mtakatifu huyo, wakati watalii wamekuwa wakipiga picha kando yake.


Lakini Papa Francis, Askofu wa zamani wa mji mkuu huo wa Argentina, aliripotiwa kutishwa na habari hizo.
Alipiga simu moja kwa moja na kutoa maneno makali kwa padri huyo aliyehusika akimweleza: "Angusha hicho kitu, haraka", gazeti la Argentina la Clarin liliripoti.
Vyanzo vya kanisa vililieleza gazeti hilo kwamba Papa Francis amedhamiria kuepuka kutengeneza 'upendo wa ubinafsi' kama ule aliofurahia Papa John Paul II.
Tangu alipochaguliwa mwezi Machi, Papa Francis amefika mbali kuonekana kama asiyetaka makuu, akionesha uvumilivu kidogo kwa ufahari na msukosuko unaokuja na nafasi yake kama kiongozi wa Wakatoliki bilioni 1.2 kote duniani.
Mara chache huvaa joho na mapambo ya kitamaduni maalumu kwa Papa huyo, na kuendelea badala yake kuvalia kanzu ya kawaida nyeupe na msalaba wa chuma.
Amegoma kuhamia kwenye makazi ya kifahari ya Papa, akisema ni makubwa mno, na kupenda kuishi badala yake katika nyumba ya kawaida ya wageni kwa ajili ya watawa wanaokuja kutembelea Vatican., ambao pamoja nao hula chakula na kuendesha misa kila siku asubuhi.
Lakini umaarufu wake mpya hauepukiki - hasa kuondoshwa kwa sanamu hiyo kugongana na kutajwa kwa Francis kama Mwanaume Bora wa Mwaka na jarida la Vanity Fair lililochapishwa Italia.
Jarida hilo lilisema:
"Siku zake 100 tayari zimemweka kwenye kundi la viongozi wa dunia walioweka historia. Lakini mapinduzi yanaendelea..."
Sanamu hiyo, iliyosimikwa siku kumi zilizopita, ilikuwa ni mtazamao wa mchongaji Fernando Pugliese, ambaye pia alitengeneza sanamu bustani ya wazo Katoliki inayoitwa Holy Land (Ardhi Takatifu) nchini Argentina. Hapo awali alishawahi kutengeneza sanamu za Papa John Paul II na Mama Teresa.
Inasubiriwa kuona kama makumbusho ya Papa Francis kwenye eneo hilo, yaliyotangazwa wiki mbili zilizopita, nayo yatapigwa marufuku na Papa huyo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog