Friday, December 18, 2015


Meneja wa bidhaa wa benki ya Barclays Tanzania, Valence Luteganya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuzindua kampeni ya matumizi ya Kadi za VISA za benki ya Barclays kwaajili ya wateja wake. Pia Lutenganya amesema kuwa kampeni hii itadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Desemba 17 mwaka huu hadi Februari 28, 2016. Kampeni hii itamwezesha mteja kunufaika na mafao mbalimbali yanayohusiana na malipo kabla na baada ya kutumia kadi zao za Visa. Wateja wenye kazi hizo wanaweza kunywa na kula kwa bei ya punguzo kwenye toteli zilizopo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkuu wa kitengo cha Masoko wa benki ya Barclays, Joe Bendera.
Mkuu wa kitengo cha Bidhaa katika benki ya Barclays, Oscar Mwamfwagasi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kuzindua kampeni ya matumizi ya Kadi zake za VISA kwaajili ya wateja wa benki hiyo. Pia amesema kuwa punguzo la bei itakuwa katika hoteli ya Southen Sun na Double Tree by Hilton, ambapo huduma za kadi za VISA za benki hiyo, wateja wenye kazi hizo watapata ofa kwa huduma yeyote kwa punguzo la 10% katika huduma za maeneo tofauti tofauti kama hoteli ya Double Tree by Hilton jijini Dar es Salaam, Double Tree by Hilton Zanzibar Nungwi, Double Tree by Hilton Stone Town- Zanzibar, Bayt El Salaam-Ston Town Zanzibar na Hoteli ya Southern Sun- Dar es Salaam kwa punguzo la 20% mpaka 30%.

Wateja wanaweza kazi zao za Barclays kwaajili ya malipo ya huduma malimbali katika maduka ya ndani ya nchi na Nje ya nchi na kutoa pesa kwenye ATM za ndani na nje ya nchi.Kutoka kulia ni Kaimu Mkuu wa kitengo cha Masoko wa benki ya Barclays, Joe Bendera, Meneja wa bidhaa wa benki ya Barclays Tanzania, Valence Luteganya na Meneja wa bidhaa wa benki ya Barclays, Erica Mwaipopo.

Kutoka kulia ni Kaimu Mkuu wa kitengo cha Masoko wa benki ya Barclays, Joe Bendera, Meneja wa bidhaa wa benki ya Barclays Tanzania, Valence Luteganya, Mkuu wa kitengo cha Bidhaa katika benki ya Barclays, Oscar Mwamfwagasi na Meneja wa bidhaa wa benki ya Barclays, Erica Mwaipopo wakionyesha kadi za VISA za benki ya Barclays mara baada ya kuzindua kaDi hizo jijini Dar es Salaam leo.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog