Thursday, June 4, 2015


Steve McClaren anatarajiwa kuthibitishwa kuwa Meneja mpya wa Klabu ya Ligi Kuu England Newcastle Wiki ijayo.
McClaren, mwenye Miaka 54, ni Meneja wa zamani wa England na pia aliwahi kuwa Meneja Msaidizi chini ya Sir Alex Ferguson huko Manchestet United.
Mwezi uliopita McClaren alutimuliwa kama Kocha wa Derby County inayochezea Ligi ya chini Championship.
Mara mbili McClaren amewahi kuigomea Newcastle kuwa Meneja wake na mara ya kwanza ilikuwa Desemba iliyopita wakati Alan Pardew alipoondoka na mara ya pili ni wakati Newcastke wakibakisha Mechi 3 za Ligi Msimu ulioisha Mei huku wakiwa hatarini kuporomoka Daraja lakini mwishoni walipona baada ya kuipiga West Ham 2-0 Siku ya mwisho ya Ligi.
Tangu alipoondoka Alan Pardew Newcastle ilikuwa chini ya John Carver ambae nae aliomba kushika wadhifa wa Meneja lakini sasa ameukosa lakini amebakishwa kama mmoja wa Makocha wa Klabu hiyo.

Mmoja wa wengine waliowania kuwa Meneja Newcastle ni Mchezaji wa zamani wa Newcastle Patrick Viera ambae hata hivyo alitoka mapema kwenye kinyang'anyiro baada ya kutoafikiana kuhusu masuala ya Uhamisho na Ununuzi wa Wachezaji.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog