Wednesday, March 11, 2015


eto 
Ishu ya ubaguzi wa rangi kwa nchi za wenzetu bado imeendelea kuonekana kuchukua nafasi, hata katika soka matukio ya ubaguzi kwa baadhi ya wanasoka ambao ni weusi imeendelea kuchukua headlines.
Tukio la hivi karibuni la mashabiki wa Chelsea lilionyesha dhahiri kwamba bado hawana mapenzi na watu wa rangi nyeusi baada ya kumzuia shabiki mwenzao asipande ndani ya treni kutokana na kuwa mweusi.
etoo 
Mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Samuel Etoo ameweza kutunukiwa tuzo ya kupambana na ubaguzi wa rangi juzi jumatatu na Shirika lisilo la kiserikali la usuluhishi linalojulikana kama The European Council on Tolerance and Reconciliation (ECTR).
Mchezaji huyo raia wa Cameroon amefanikiwa kutwaa tuzo hiyo baada ya kupambana na mambo yanayohusu ubaguzi kwa kipindi chote ambacho amekuwa akicheza katika klabu mbalimbali za soka na hivi karibuni alilaani kitendo cha mashabiki wa chelsea kumbagua shabiki mwenzao kutokana na kuwa ni mtu mweusi wakati wakitoka uwanjani.
raci 
Etoo ambaye kwa sasa anaitumikia klabu ya Sampdoria alipewa tuzo hiyo ya heshima na Shirika lisilo la kiserikali la The European Council on Tolerance and Reconciliation (ECT

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog