Monday, March 2, 2015


Kocha wa Juve Massimiliano Allegri APAGAWA Baada ya timu yake kutoka sare
Ndani ya Uwanja wa  Stadio Olimpico usiku huu ilishindukana  kutoa mshindi baada ya Wenyeji AS Roma kutoka Sare na Juventus ya Bao 1-1 kwenye Mechi ya Ligi Serie A.
Matokeo hayo yameifanya Juve iendelee kuongoza Ligi hiyo ya Italy ikiwa Pointi 9 mbele ya Timu ya Pili AS Roma.
Juve walifunga Bao lao kwa Frikiki ya Dakika ya 64 iliyotolewa baada ya Vasilis Torosidis kumchezea Rafu Vidal na Beki huyo wa AS Roma akapewa Kadi Nyekundu.
Licha ya kucheza Mtu 10 AS Roma walisawazisha Dakika ya 78 kwa Kichwa cha Seydou Keita alieunganisha Frikiki ambacho kilimgonga Marchisio na kutinga.

VIKOSI:
Juventus XI (3-5-2)
Buffon, Caceres, Bonucci, Chiellini, Evra, Lichtsteiner, Vidal, Marchisio, Pereyra, Tevez, Morata.
Roma XI (4-3-3)
De Sanctis, Torosidis, Manolas, Mapou, Cholevas, Pjanic, De Rossi, Keita, Gervinho, Totti, Ljajic

Patashika kipindi cha kwanza ambapo Timu zilienda mapumziko zikiwa 0-0.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog