Monday, March 2, 2015


Jose Mourinho ameelezea nia yake kutwaa Mataji mengine mara baada ya Jana Uwanjani Wembley Jijini London Timu yake Chelsea kuichapa Tottenham Hotspur Bao 2-0 na kubeba Capital One Cup likiwa ni Kombe lake la kwanza tangu arejee kwa mara ya pili Klabuni Chelsea.
Bao za Chelsea hapo Jana zilifungwa na Nahodha John Terry na Kyle Walker aliejifunga mwenyewe.kiongea mara baada ya Mechi hiyo, Jose Mourinho alisema: “Mie ni kama mtoto alieshinda mara ya kwanza. Ni ngumu kwangu kuishi bila Mataji. Nahitaji kutwaa Makombe!”
Mourinho, ambae alikuwa Chelsea kwa mara ya kwanza kati ya Miaka 2004 na 2007 na kurejea 2013, sasa ameshatwaa Vikombe 7 akiwa na Chelsea.
Chelsea hivi sasa wanaongoza Ligi Kuu England wakiwa Pointi 5 mbele ya Mabingwa Watetezi Manchester City huku wakiwa wamecheza Mechi 1 pungufu.

CAPITAL ONE CUP
WASHINDI WALIOPITA:

1961 - Aston Villa
1962 - Norwich City
1963 - Birmingham City
1964 - Leicester City
1965 - Chelsea
1966 - West Bromwich Albion
1967 - Queens Park Rangers
1968 - Leeds United
1969 - Swindon Town
1970 - Manchester City

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog