Wednesday, September 3, 2014



https://24tanzania.com/wp-content/uploads/2014/03/65df1bcd23_Mbwana-Samatta.jpg

Waswahili hawaishiwi vioja kwa tungo, nahau, mafumbo, methali hata vitendawili. Yote yanaakisi maisha ya jamii pana inayotuzunguka. Kwa leo nimeguswa na msemo usemao, nabii hakubaliki kwao.
Nimesimama peke yangu nikiamini kuwa wapo manabii ambao wanakubalika kwao. Utakubaliana nami kuwa kiwango alichonacho Mbwana Samatta hakuna mtanzania asiyekikubali. Kwa sasa Samatta ndiye chachu na roho ya Tp mazembe. Huwezi kumwambia kitu Moses Katumbi juu ya kijana huyu wa kitanzania.
Anaibeba timu kwa uwezo wake baada ya kuondoka Tresor Mputu aliyetimkia nchini Angola, sasa hakuna kama Samatta . Ukipita kwenye viunga vya mji wa Lubumbashi vijana wanapendeza kwa jezi ya Samatta. Timu yetu ya Taifa Stars jumapili hii iko dimbani kucheza na timu ya Taifa ya Burundi. Ni siku ambayo nabii ata zidhirisha unabii wake. Naamini sasa ni wakati wa Mbwana Samatta kuibeba Taifa Stars.
Tanzania imejaliwa kuwa na vipaji vingi katika medani mbalimbali, lakini kukosekana mipango thabiti na uthubutu miongoni mwa wachezaji ni tatizo katika kupata wachezaji wa kulipwa. Wenzetu Kenya wana nyota kadhaa wanaosukuma kandanda barani Ulaya.
Kama vile kwa Waganda ambao nao hawako nyuma, kwetu Samatta atabaki kuwa kioo cha taifa kwenye mpira wa miguu . Mechi ya jumapili itaamuliwa na ubora wa Mbwana Samatta. Kila la heri Taifa Stars kwenye mchezo huo wa kirafiki ulio kwenye kalenda ya shirikisho la soka duniani Fifa. Uzalendo wetu ni silaha tosha ya kuiangusha Burundi nyumbani kwao.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog