Monday, July 28, 2014


 
index
*Msafiri Diouf, Amigolas wa Bendi ya Ruvu Stars kupamba shindano
Na Mwandishi Wetu
Wakati warembo 14 wanaowania taji la Kanda ya Mashariki ( Redds Miss Eastern Zone 2014)  (kesho Jumanne)  watashindana kwenye taji la vipaji (talent award), bendi mpya inayokuja juu kwa kasi, Ruvu Stars chini ya nyota Msafiri Diouf na Hamis Amigolas watapamba shindano hilo lililopangwa kufanyika  kwenye ukumbi wa Maisha Plus, Kibaha, Mkoa wa Pwani.
Akizungumza jijini jana, mratibu wa mashindano hayo, Alex Nikitas alisema kuwa awali walipanga kufanya shindano hilo siku ya Idd Pili, lakini kutokana na muda wameamua kulifanya leo ili kuwapa muda zaidi warembo kwa ajili ya mazoezi ya kuwania taji la mrembo wa Kanda ya Mashariki Agosti 8 kwenye hotel ya Nashera mkoani  Morogoro.
Nikitas alisema maandalizi ya shindano hilo yamekamilika na onyesho litaanza saa 2.00 usiku huku warembo wakichuano katika vipaji mbalimbali kama kuimba, kucheza muziki wa kisasa, wa asili na ya nje ya nchi. Alisema kuwa mgeni rasmi katika shindano hilo ni Mbunge wa Kibaha mjini, Silvester Koka.
“Warembo wapo katika maandalizi makali  tayari kuchuana katika mashindano hayo, mbali ya vipaji, pia warembo hao watatoa misaada mbalimbali kwa vituo vya watoto yatima katika mkoa huo,” alisema Nikitas.
Alisema kuwa warembo hao wataondoka mkoa wa Pwani Julai 31 tayari kwa kambi ya mwisho kwenye hotel ya Usambara Safari Lodge chini ya Miss Kanda ya mashariki wa mwaka jana,  Diana Laizer.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog