Friday, July 25, 2014

article-2704976-1FE959CE00000578-364_634x435Tumelianzisha tena! Raheem Sterling anajua wazi kuwa anatakiwa kujithibitsha mwenyewe kuwa ni bora.
LICHA ya kuwa miongoni mwa wachezaji wachache wa England waliorudi na heshima kutoka kombe la dunia, Raheem Sterling amesisitiza kuwa anahitaji kuonesha kiwango kikubwa katika klabu yake ya Liverpool msimu ujao.
Nyota huyo kinda mwenye miaka 19 alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Liverpool waliokaribia kutwaa ubingwa wa ligi kuu ambapo walimaliza pointi mbili nyuma ya mabingwa Manchester City.
article-2704976-1FE4034B00000578-925_634x435 
Kivutio: Raheem Sterling amekuwa na mvuto tangu alipowasili katika kambi ya Liverpool iliyopo Boston.
Sterling amejiunga na kambi ya mazoezi iliyopo Boston akijua wazi kuwa kusajiliwa kwa wachezaji wapya kunamaanisha nafasi yake haina uhakika.
Akizungumza na LFCTour.com, alisema: “Bado natakiwa kujithitisha mwenyewe, kocha ameleta wachezaji ambao wenye uwezo wa kucheza nafasi kama yangu, natakiwa kumuonesha kocha na kujituma zaidi ili kupata namba ya kudumu katika timu”.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog