Friday, May 9, 2014


Lionel-Messi-v-Athletic-Bilbao_3128305LIONEL Messi amechukizwa na tabia ya vyombo vya habari kuzungumzia hatima yake katika klabu ya Barcelona na kusisitiza kuwa hawatachia taji la La Liga msimu huu.
Tetesi zilizoenea katika vyombo vya habari nchini Hispania zinasema kuwa nyota huyo raia wa Argentina anaweza kuondoka Camp Nou.
Messi aliyeshinda mataji sita ya La Liga na matatu ya UEFA amesisitiza kuwa ana furaha kubwa Barcelona na hataondoka majira ya kiangazi.
Hata hivyo kuna taarifa kuwa siku chache zijazo Messi atasaini mkataba mpya utakaomuweka kwa wakatulanya hao mpaka mwaka 2019.
Nyota huyo mwenye miaka 26 amejiweka mbali na tetesi hizo na kusisitiza kuwa kwasasa anafikiria namna ya kuisaidia Barcelona kushinda mechi zake mbili zilizosalia msimu huu.
Messi amekaririwa na gazeti la Marca, akisema: “Wamesema mambo mengi kwa mwaka huu”.
“Habari nyingi zimezungumzwa, nyingi ni uongo. Niko sawa”.
“Kwasasa tumekuwa nafasi nzuri zaidi ,” aliongeza Messi. “Tunaona uwezekano wa kubeba taji upo, lakini itategemeana tutafanya nini”.
“Tutaitumia nafasi hii na hatutaiacha iende”.
Barcelona wamebakiza mechi dhidi ya Elche na vinara Atletico Madrid.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog