Thursday, December 26, 2013


Kama tulivyowaahidi wasomaji wetu wa  http://www.bongo123.com/ (Bongonewz Magazine) kuwa leo tutatoa matokeo ya mpampano ambao tuliuanzisha juzi tarehe 24 December. Tulimpambanisha ALLY KIBA na Diamond platnumz kupitia ukurasa wetu wa Facebook kwa kuweka picha na watu kucomment jina la msanii wanayemkubali >>>>TAZAMA HAPA<<<. Mbali na ukurasa wa facebook, pia wasomaji walipiga kura kupitia mtandao huu >>>HAPA<<<<.  Mpambano ulikuwa mkali na wasanii hawa walivutana kweli lakini mwisho wa siku matokeo yalikuwa hivi!!!
KATI YA KURA 159 ZILIZOPIGWA KUPITIA FACEBOOK NA KATIKA MTANDAO HUU MATOKEO YALIKUWA HIVI:
ALLY KIBA ==============KURA 110
DIAMOND PLATNUMZ======KURA 43
ZILIZOHARIBIKA==========KURA  6
Kutokana na matokeo haya, wasomaji wengi wameonyesha kumkubali zaidi ALLY KIBA kuliko Diamond kwani amemzidi sana Diamond kwa kura, na baadhi ya wasomaji walitoa maoni yao kuwa  Diamond ana nyota tu lakini hajui kuimba kama Ally Kiba na kwamba anajua sana kuuza skendo ndio maana amekuwa akisikika sana. Japokuwa Ally Kiba yupo kimya lakini mziki wake unakubalika zaidi
SASA HII NI CHANGAMOTO KWA ALLY KIBA KUTOA VITU VITAKAVYOENDELEA KUMUWEKA JUU NA HATIMAYE KUMFUNIKA ZAIDI DOGO DIAMOND.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog