Friday, March 31, 2017


VPL, LIGI KUU VODACOM, inarejea tena kwa kishindo Jumamosi hii Aprili Mosi kwa Mechi 3 na kubwa kabisa ni ile itayopigwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kati ya Mabingwa Watetezi Yanga na Timu ngumu Azam FC.
Hakika Mechi hii ni Bigi Mechi na itatoa mwanga mkubwa kama kweli Yanga wanaweza kutetea Ubingwa wao hasa kwa vile wapo Nafasi ya Pili wakiwa Pointi 2 nyuma ya Vinara Simba huku wote wakiwa wamecheza Mechi 24 kila mmoja na kubakiza Mechi 6 tu kila mmoja.

Azam FC wao wapo Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 9 nyuma ya Yanga wakiwa bado wana matumaini finyu ya Ubingwa.

Mechi nyingine za hiyo Jumamosi, ambazo hasa nyingi ni vita za kutoshuka Daraja, ni huko Songea kati ya Maji Maji FC na Toto Africans wakati nyingine ni Mjini Mbeya kati Mbeya City na Ruvu Shooting.

Jumapili zipo Mechi 4 na Macho Kodo ni huko Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba kati ya Kagera Sugar, walio Nafasi ya 4, wakiwavaa Vinara Simba.

Nyingine za Jumapili ni Jijini Dar es Salaam kati ya African Lyon na Stand United, Mjini Mbeya ni Tanzania Prisons na Mtibwa Sugar na huko Mwadui Complex, Shinyanga ni Mwadui FC na JKT Ruvu.

VPL – LIGI KUU VODACOM
Jumamosi Aprili 1

Yanga v Azam FC
Maji Maji FC v Toto Africans
Mbeya City v Ruvu Shooting

Jumapili Aprili 2

Kagera Sugar v Simba
African Lyon v Stand United
Tanzania Prisons v Mtibwa Sugar
Mwadui FC v JKT Ruvu

Jumamosi Aprili 8
Stand United v Tanzania Prisons
Kagera Sugar v JKT Ruvu
Yanga v Toto Africans
Mtibwa Sugar v Azam FC

Jumapili Aprili 9
Mbeya City v Ndanda FC
Maji Maji FC v African Lyon

Jumatatu Aprili 10
Mbao FC v Simba

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog