Friday, March 31, 2017


Kiungo wa kimataifa wa Hispania anayeichezea Man United ya England Juan Mata jina lake limerudi kwenye headlines baada ya kufanyiwa upasuaji wa groin, Mata ambaye mwanzoni mwa wiki hii alikuwa akilalamika mazoezini kuwa anasumbuliwa na groin amefanyiwa upasuaji.
Taarifa zilizotoka usiku wa March 31 2017 kuhusu kiungo huyo ni kuwa upasuaji wake umeenda salama lakini kutokana na tatizo lake, kuna uwezekano mkubwa wa kukosa mechi zote za kumalizika za Man United tofauti na awali alivyotazamiwa kuwa anaweza kukosa mechi tatu tu.

Juan Mata ambaye alijiunga na Man United akitokea Chelsea mwaka 2014 , hajawahi kukosa mechi za Man United katika kipindi cha miaka yote mitatu aliyokuwepo klabuni hapo pasipokuwa na majeruhi, mara zote amekuwa akikosekana kwa sababu za msingi ikiwemo majeruhi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog