Tuesday, October 27, 2015

Muigizaji Kingwendu ni miongoni mwa mastaa ambao wamechukua headline za kugombea Ubunge kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kama Afande Sele, Professor Jay, Muigizaji Frank na wengineo.
Stori iliyonifikia ni kwamba muigizaji huyo hakufanikiwa kupata Ubunge kupitia tiketi ya CUF katika  jimbo la Kisarawe mkoa wa Pwani.
Akiongea na ripota wa millardayo.com alisema…’Matokeo ya mwanzo yalikuwa yanaonesha kwamba mimi naongoza, lakini mwishoni katika hesabu ikaonekana amenishinda‘- KINGWENDU
‘Matokeo yanaonesha Suleimani Jako wa CCM ameshinda, nimejaribu na nimethubutu kwa mara ya kwanza..! najua nimekosea wapi na ntajipanga upya na ntaenda kusomea siasa zaidi’– KINGWENDU
‘Hakuna mtu aliyenishawishi kugombea ubunge, bali ni mimi mwenyewe niliamua baada ya kuona pia baadhi ya wasanii wenzangu wanagombania‘-KINGWENDU

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog