Sunday, August 2, 2015


maxresdefault
Kuelekea kuanza kwa Ligi Kuu Ujerumani Bundesliga August 1 imepigwa mechi ya Fainali ya Super Cup, mchezo huo ulizikutanisha timu za FC Bayern Munchen dhidi ya klabu ya Wolfsburg katika uwanja wa Volkswagen Arena.
Generated by  IJG JPEG Library
Mchezo umemalizika kwa Wolfsburg kuibuka washindi baada ya dakika 90 za mchezo kumalizika kwa sare ya goli 1-1, hadi dakika ya 88 FC Bayern Munchen walikuwa wanaongoza kwa goli 1-0 goli lililofungwa na Arjen Robben dakika ya 47 ya mchezo kabla ya Nicklas Bendtner kufunga goli la kusawazisha dakika 89 kwa upande wa Wolfsburg.
482661198
Kevin De Bruyne akiwa na tuzo ya mchezaji bora wa mwaka

Hivyo ikalazimika kupigwa mikwaju ya penati ambapo Wolfsburg wakaibuka na ushindi kwa jumla ya penati 5-4 kwa upande wa FC Bayern Munchen kiungo wa Kihispania Xabi Alonso alikosa penati. Sambamba na hayo kiungo wa kimataifa wa Ubeligiji Kevin De Bruyne alipata tuzo ya mchezaji bora wa mwaka inayotolewa na waandishi wa habari za michezo Ujerumani.
Pichaz na Video nimekusogezea mtu wangu


Generated by  IJG JPEG Library



Generated by  IJG JPEG Library



482661198

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog