Tuesday, July 7, 2015


Raia huyo wa Uingereza ambaye harakati za kuhamia Manchester City, zilitumbukia nyong'o amekadiriwa kuwa mwenye thamani ya pauni milioni 35 na kampuni ya utafiti ya Soccerex inayochapisha Orodha ya wachezaji wenye thamani ya juu ama 20 Football Value Index.
Manchester City ilikuwa imeweka dau la pauni milioni £40 lakini ombi lao likakataliwa na Liverpool.
Mlinzi wa Manchester United, Luke Shaw ameorodheshwa katika nafasi ya 9, John Stones wa Everton ameorodheshwa wa 16 huku kiungo wa Arsenal Calum Chambers akiorodheshwa katika nafasi ya 19.

Kampuni hiyo ya Soccerex imefanya utafiti huo miongoni mwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 wanaocheza katika ligi za bara ulaya.
Inatumia vipengee kama umri,nafasi wanayocheza uwanjani,Klabu,urefu wa Kandarasi,mechi walizochezea timu zao za taifa,mechi walizocheza,mabao waliofunga,majeraha na ubora wao kitalanta.

''tukiangalia kwa kina vipengee hivi vyote tunaweza kutathmini uwezo na thamani ya mchezaji.''
''Hivyo vyote ndivyo vilitusaidia kubaini kuwa Sterling ndiye mchezaji bora na mwenye thamani ya juu zaidi barani ulaya kwa sasa.'' alisema bwana Esteve Calzada
Mlinzi wa Paris St-Germain ya Ufaransa ambaye ni raia wa Brazil Marquinhos ameorodheshwa katika nafasi ya pili na thamani ya pauni milioni £27.8.
Mchezaji mpya wa Manchester United vilevile ye Uingereza Memphis Depay aliyegharimu kitita cha pauni milioni £31 ameorodheshwa katika nafasi ya tatu akiwa na thamani ya pauni milioni £23.8.

Calzada anasema kuwa sheria iliyowekwa na shirikisho la soka la Uingereza ambayo inazilazimisha vilabu vya Uingereza kuwa na takriban wachezaji 8 raia wa Uingereza imeongeza maradufu thamani ya wachezaji waingereza.
Wachezaji 4 katika orodha hiyo ni raia wa Uingereza huku 9 kati ya 20 bora wakitarajiwa kucheza katika ligi kuu ya Uingereza msimu ujao.


RAHEEM STERLING AKILINGANISHWA NA WENGINE HAPA!

1. Raheem Sterling (Liverpool) £35m 7. Mateo Kovacic (Inter Milan) £18.5m
2. Marquinhos (Paris St-Germain) £27.8m 8. Jose Gaya (Valencia) £18.3m
3. Memphis Depay (Manchester United) £23.8m 9. Luke Shaw (Manchester United) £18m
4. Domenico Berardi (Sassuolo) £21.6m 10. Aymeric Laporte (Athletic Bilbao) £17m
5. Jose Gimenez (Atletico Madrid) £21.4m 16. John Stones (Everton) £12m
6. Hakan Calhanoglu (Bayer Leverkusen) £19.4m 19. Calum Chambers (Arsenal) £10.6m

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog