Thursday, July 2, 2015


Bayern Munich wamemsaini Kiungo kutoka Brazil Douglas Costa aliekuwa Shakhtar Donetsk ya Ukraine.
Costa, mwenye Miaka 24, amelipiwa Ada ya Uhamisho ya Pauni Milioni 21 na kusaini Mkataba wa Miaka Mitano.
Kusainiwa kwa Costa huenda kukafungua njia kwa Kiungo Mkongwe Bastian Schwensteiger, mwenye Miaka 30, kuhamia Manchester United kwa vile sasa Kocha Pep Guardiola, ambae Msimu uliopita aliiongoza Bayern kutwaa Taji lao la 25 la Bundesliga, ana utitiri wa Viungo wakiwemo Franck Ribery wa France, na Wachezaji wa Spain Thiago Alcantara, Xabi Alonso na Javi Martinez.
Hivi sasa Schweinsteiger hachezi mara kwa mara kwenye Timu ya Bayern na Msimu uliopita alicheza Mechi 20 tu za Ligi ikiwa ni idadi ndogo kabisa tangu aanze kuichezea Bayern mwaka 2002.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog