Wednesday, September 24, 2014

Edu Albácar ndie aliyeanza kuifunga Real bao dakika ya 15 bao la mkwaju wa penati.
Gareth Bale hakuchukua muda dakikia 20 alisawazisha bao la hilo kwa kichwa na kufanya 1-1.
Cristiano Ronaldo alifunga bao la pili dakika ya 28 na kufanya 2-1 na baadae dakika ya 32 akaifungia bao tatu na kufanya 3-1 dhidi ya Elche kwenye Uwanja wa Nyumbani Bernabeu na ukishuhudiwa na Mashabiki 65,000.
Bao zote tatu zikifungwa katika kipindi cha kwanza cha dakika 45.
Kipindi cha pili dakika ya 80 Cristiano Ronaldo alifunga hat-rick kwa kufunga bao la nne na kufanya bao kuwa 4-1 dhidi ya Elche.

Ronaldo tena katika dakika za majeruhi alitupia bao lingine la tano na kuhitimisha mpira huo Real wakiwa na bao 5-1 dhidi ya Elche baada ya Ronaldo kupata pasi kutoka kwa Gareth Bale.


Fowadi wa Elce  Edu Albscar akishangilia bao lake la mkwaju wa penati

Bale aliweka sawa mambo kwa kufanya 1-1 nyumbani Bernabeu

Ronaldo akaipachikia bao la pili na kufanya 2-1

Ronaldo akishangilia bao lake la kuhitimisha Hat-trick yake leo hii usiku 
Ronaldo akifunga moja ya bao lake leo hii kwa kichwa

Ronaldo akishangilia bao lake

Sergio Ramos kwenye patashika!

Baadhi ya Wachezaji wa Real wakimpongeza mwenzao Staa Ronaldo

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog