Sunday, August 24, 2014

 


Taswira kamili Uwanja wa taifa Jijini Dar es selaam.
MBELE ya Rais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, Leo kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Malejendari wa Real Madrid waliwachapa wenzao wa Tanzania Bao 3-1 kwenye maalum ya Kirafiki iliyohudhuriwa na Washabiki wengi.
Bao zote za Real zilifungwa na Kiungo wao wa zamani Reuben de La Red, mwenye Miaka 29, ambae alilazimika kustaafu Soka Mwaka 2010 baada ya kupata matatizo ya Moyo.
Bao pekee la Tanzania lilikuwa ni la kujifunga wenyewe Real kupitia Roberto Rojas.
Mechi hii ya Kirafiki ilipambwa hasa na Mkongwe Luis Figo ambae aling’ara na kwenye Kiungo cha Real, Christian Karembeu, alionyesha bado wamo.
Kwa upande wa Tanzania Makipa Mohammed Mwameja, aliecheza Kipindi cha Kwanza, na Peter Manyika, aliecheza Kipindi cha Pili, walionyesha ustadi wao lakini ni Kali Ongala ndie alikuwa Nyota kwa Mpira wake wa akili.
Hadi Mapumziko, Timu hizi zilikuwa Sare kwa Bao 1-1.
Kipindi cha Pili, Real walipiga Bao 2 zaidi na moja likiwa Penati iliyosababishwa na Habib Kondo.Mdau wa bukobasports.com Willy Kiroyera (kulia, akiwa ametokelea akiwa na marafiki zake wakiwa tayari kushuhudia kipute cha Tanzania Eleven na Magwiji wa Real Madrid leo Kipute kikiendelea Uwanjani kipindi cha kwanza ambapo Tanzania walikuwa sare ya 1-1Nyomi...Mashabiki walijitokeza kwa wingi kushuhudia kipute hicho kilichomalizika kwa bao 3-1 Tanzania wakichapwa na Mchezaji mmoja wa Real aliyetupia hat-trick. Moja likifungwa kwa mkwaju wa penati.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog