Friday, July 4, 2014

RAIS mpya wa Klabu ya Simba, Evans Aveva, ameanza kazi yake rasmi kwa kuteua Kamati mbalimbali za Klabu hiyo na pia kusimamisha Wanachama 69 waliofungua Kesi Mahakamani.
Aveva alitinga madarakani Simba baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumapili iliyopita Jijini Dar es Salaam kwa kuzoa Kura 1455 na kumshinda Andrew Tupa aliepata Kura 388.
Makamu wa Rais alichaguliwa Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliepata Kura 1046 na kuwabwaga Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ aliepata Kura 412, Swedi Nkwabi, Kura 373 na Bundala Kabula. 25.
Wajumbe wa Kamati Kuu waliochaguliwa kwenye Uchaguzi huo ni Idd Kajuna, Said Tully, Collins Frich, Ally Suru na Mwanamama Jasmine Badour.

Mbali ya Wajumbe hao, Rais Aveva, akitumia mamlaka yake Kikatiba, ameteua Watu watatu kuingia kwenye Kamati Kuu ambao ni Mohammed Nassor, Musleh Al Ruwaih na Salim Abdallah.
Kikao cha kwanza kabisa cha Kamati Kuu kiliamua kuwasimamisha Wanachama 69 ambao waliwasilisha Kesi Mahakamani kutaka kusimamisha Uchaguzi Mkuu na uamuzi wa hatima yao pamoja na ya Michael Wambura, aliezuiwa kugombea kwenye Uchaguzi, utatolewa na Mkutano Mkuu wa Simba utakaofanyika Agosti 3.



KAMATI ALIZOTEUA RAIS AVEVA:
KAMATI YA USAJILI

-Zacharia Hans Pope

- Mwenyekiti
-Kassim Dewji
-Dr Rodney Chiduo
-Musleh Al Ruwaih
-Crescentius Magori
-Said Tully

KAMATI YA VIJANA
-Said Tully - Mwenyekiti
-Ally Suru
-Patrick Rweyemamu
-Mulamu Nghambi
-Amina Poyo
-Madaraka Suleiman

KAMATI YA MASHINDANO

-Mohammed Nassor 

– Mwenyekiti
-Iddi Kajuna
-Jerry Yambi
-Hussein Simba

 -Mohammed Omar

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog