Tuesday, May 13, 2014


404372_heroaCARLOS Tevez ameachwa kwenye kikosi cha awali cha kocha  wa Argentina,  Alejandro Sabella kwa ajili ya kombe la dunia mwezi ujao nchini Brazil.
Mshambuliaji huyo wa  Juventus licha ya kuonesha kiwango kizuri katika ligi ya Seria A, bado hajamshawishi Sabella kuingizwa katika kikosi cha timu ya taifa kinachojiandaa kwenda nchini Afrika kusini.
Franco Di Santo, Rodrigo Palacio na nahodha Lionel Messi wataongoza safu ya ushambuliaji, wakati huo huo mchezaji anayecheza kwa mkopo, Atletico Madrid ,  Jose Sosa  ameitwa katika kikosi hicho.
Kikos kizima hiki hapa:
Walinda mlango: Sergio Romero (Monaco*), Mariano Andujar (Catania*), Agustin Orionu (Boca)
Walinzi: Ezequiel Garay (Benfica), Federico Fernandez (Napoli), Pablo Zabaleta (Manchester City), Marcos Rojo (Sporting), Jose Maria Basanta (Monterrey), Hugo Campagaro (Inter), Nicolas Otamendi (Atletico Mineiro*), Martin Demichelis (Manchester City), Gabriel Mercado (River), Lisandro Lopez (Getafe*)
Viungo: Fernando Gago (Boca*), Lucas Biglia (Lazio), Javier Mascherano (Barcelona), Ever Banega (Newell’s*), Angel Di Maria (Real Madrid), Maximiliano Rodriguez (Newell’s), Ricardo Alvarez (Inter), Augusto Fernandez (Celta), Enzo Perez (Benfica), Jose Sosa (Atletico Madrid*), Fabian Rinaudo (Catania)
Washambuliaji: Sergio Aguero (Manchester City), Lionel Messi (Barcelona), Gonzalo Higuain (Napoli), Ezequiel Lavezzi (Paris Saint-Germain), Rodrigo Palacio (Inter), Franco Di Santo (Werder Bremen)

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog