Friday, December 20, 2013


 
Share
MASHABIKI wa Liverpool huenda wakachekelea kwa muda kukalia usukani endapo timu yao itaichapa Cardiff City mchana wa leo Jumamosi.
Arsenal inaongoza Ligi Kuu England ikiwa na pointi 35 lakini Liverpool na Chelsea itakayocheza keshokutwa Jumatatu na Arsenal wote wana pointi 33.
Potezea hiyo, ngoma ipo kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam jioni hii. Kuna mechi matata ya Nani Mtani Jembe kati ya Simba na Yanga ambao ni mchezo wa kujifurahisha lakini uliobeba uzito wa aina yake kishabiki.
Simba inashuka uwanjani ikijivunia majembe yake mapya ambayo ni makipa, Yaw Berko, Ivo Mapunda, kiungo, Awadhi Juma, straika Ally Badru na beki Donald Musoti lakini kama haitoshi, Wekundu hao wana kocha mtaalamu na mwenye mbwembwe za aina yake Zdravko Logarusic kutoka Croatia.
Ndani ya kambi ya Simba mjini Zanzibar mambo yalikuwa shwari wiki nzima huku wakipigishwa tizi mara mbili kwenye Uwanja wa Fuoni.
Rudi kwa Yanga, ina vifaa vipya matata kama Juma Kaseja, Hassan Dilunga na straika aliyezua gumzo zaidi nchini baada ya kutua Jangwani, Emmanuel Okwi.
Timu hizo mbili zinakumbana zikiwa na wachezaji ambao wamewahi kuzichezea zote kwa nyakati tofauti jambo ambalo ni burudani nyingine.
Wachezaji hao kwa upande wa Yanga ni Juma Kaseja, Kelvin Yondani, Mrisho Ngassa, Ally Mustapha ‘Barthez’, Deo Munishi ‘Dida’, Athuman Idd na Okwi. Simba ina makipa Mapunda na Berko na Amri Kiemba.
KOCHA YANGA
Ernest Brandts ambaye ni kocha wa Yanga alisema; “Tumejiandaa vizuri na sasa tumebakiza dakika chache kabla ya mechi. Kiujumla timu ipo vizuri na majeruhi tuliyenaye ni Salum Telela pekee ambaye hayuko vizuri sana.”
“Ninachowaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuja kushabikia timu yao na naamini tutashinda mchezo huo bila shida,”alisema kocha huyo kwa kujiamini huku akikiri kwamba anaweza kumtumia Okwi dakika kadhaa.
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ alisema; “Tuna kila sababu ya kushinda mchezo huo, maandalizi yalikuwa mazuri na kila kitu kinakwenda sawa.”

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog