Thursday, June 25, 2015


Nathaniel Clyne yuko mbioni kujiunga na Liverpool baada ya Klabu yake Southampton kuikubali Ofa ya Pauni Milioni 12.5.
Clyne, ambae ni Fulbeki wa Kulia, anakuwa Mchezaji wa 6 kusainiwa na Liverpool katika kipindi hiki cha kuelekea Msimu mpya.
Uhamisho huu wa Clyne, mwenye Miaka 24 na ambae ameichezea England mara 5, utakamilika baada ya upimaji wa Afya yake na makubaliano ya maslahi yake binafsi.
Clyne atakuwa Mchezaji wa 4 kujiunga na Liverpool kutoka Southampton kufuatia wale waliojiunga Mwaka Jana ambao ni Adam Lallana, Dejan Lovren na Rickie Lambert.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog