Thursday, June 18, 2015


MSHAMBULIAJI wa timu ya Stand United,Abasarim Chidiebele akizungumza na waandishi wa habari mkoani Tanga mara baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia timu ya Coastal Union,Picha na Mwandishi Wetu,Tanga

MSHAMBULIAJI wa timu ya Stand United, Abasarim Chidiebele, amesaini mkataba wa kuitumikia timu ya Coastal Union kwa mkataba wa mwaka mmoja katika msimu ujao wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.
Chidiebele alitua mkoani Tanga juzi kwa ajili ya kuingia makubaliana na uongozi wa timu ya Coastal Union ambapo utiliaji saini huo ulishuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa Coastal Union, Kassim El Siagi, Meneja wa Coastal Union, Akida Machai na viongozi wengine.
Akizungumza mara baada ya kusaini, Chidiebele amesema kuwa amefurahi kusajiliwa na Coastal Union na kuhaidi kutumia uwezo wake aliokuwa nao kwa ajili ya kuipa mafanikio timu hiyo katika michuano ya Ligi kuu msimu ujao.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog