Tuesday, June 2, 2015


Meneja wa Chelsea, Jose Mourinho, amekanusha habari hizo.
Katika Msimu wake wa kwanza na Chelsea ambao ulimalizika Majuzi, Costa alipiga Bao 20 za Ligi Kuu England na kuiwezesha Klabu hiyo kutwaa Ubingwa.
Costa, ambae alijiunga na Chelsea mwanzoni mwa Msimu huu uliokwisha kwa Dau la Euro Milioni 40, hakucheza vizuri awamu ya pili ya Ligi baada ya kuundamwa na Majeruhi na Kifungo.
Akiongea hii Leo baada ya Chelsea kuifunga Sydney Bao 1-0, Mourinho alitamka: "Yeye ni Mtu anaefurahisha kwenye Timu yetu.
Ana furaha, anachekesha na anafurahia kila kitu. Kama hiyo ni kutokuwa na furaha Klabuni basi mie nasikia raha. Yeye hakufurahishwa na habari hizo."
Kwenye Mechi hiyo na Sydney FC huko Nchini Australia, Costa alicheza Dakika 40 za Kipindi cha Kwanza lakini bao pekee na la ushindi lilifungwa na Loic Remy.

Licha ya kufunga Bao 20 kwenye Ligi, Diego Costa hakufunga hata Bao moja kwenye Mashindano mengine ambayo Chelsea ilifika mpaka Fainali ya
Kombe la Ligi, Capital One Cup, na kutwaa Kombe na pia kucheza Mechi 7 za UEFA CHAMPIONS LIGI.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog