Wednesday, June 24, 2015



Mchezaji wa Yanga Juma Abdul (kulia0 akimtoka mchezaji wa Friends Rangers leo kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Karume

TIMU ya Yanga yenye maskani yake mtaa wa Jangwani na Twiga jana iliifunga Friends Rangers mabao 3-2 kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Yanga ambayo ilikuwa inawajaribu wachezaji wake ambao wamesajiliwa msimu huu ilianza kupata bao la kwanza dakika ya 11 lililofungwa na Kpah Sherman akimalizia pasi ya Busungu
Hata hivyo Friends Rangers walisawazisha bao hilo dakika ya 25 lililofungwa na Mussa Juma lakini dakika ya 37 Yanga waliongeza bao la pili lililofungwa na Busungu baada ya kupokea pasi toka kwa Sherman bao lililodumu hadi mapumziko.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog