Saturday, June 6, 2015



Luis Suarez, Neymar, Jordi Alba, Lionel Messi, Javier Mascherano na Gerard Pique kwenye mazoezi yao wiki hii wakijiandaa ya Mtanange wa Fainali ya Uefa Champions League kesho Jumamosi Juni 6, 2015.
Hii ni Fainali ya UEFA CHAMPIONS ambayo ama FC Barcelona ya Spain au Juventus ya Italy itatwaa Ubingwa wa Ulaya na pia Bingwa huyo atakuwa ametwaa Trebo Msimu huu baada ya Timu zote mbili kutwaa Makombe mawili Nchini mwao yale ya Ubingwa na Kombe la Nchi.
Habari kubwa ya Fainali hii ni kukosekana kwa ule mvuto mkubwa wa kuwakutanisha tena kwa mara ya kwanza Beki wa Juventus Giorgio Chiellini na Fowadi wa Barcelona Luis Suarez baada ya Chiellini kuumia Jumatano.
Wachezaji hao walivaana huko Brazil Mwaka Jana wakizichezea Nchi zao kwenye Fainali za Kombe la Dunia na Suarez kuadhibiwa kwa Kifungo kirefu kwa kumng'ata Meno Chiellini.

Messi kulia

Messi kwenye mazoezi akikabwa na  Dani Alves pamoja na  Adriano.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog