Tuesday, March 11, 2014

 
Basi la Kampuni ya Hood likiwa limepinduka na watu kuumia vibaya Same,Kilimanjaro chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana
. 
Mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo.
Basi la Kampuni ya Hood likiwa limepinduka na watu kuumia vibaya eneo la Same leo asubuhi

Baadhi ya wasamalia wema wakiwaokoa abiria waliokuwa wamepanda basi hilo la hood lililokuwa linatoka Arusha kwenda Mbeya baada ya kupinduka.




Ajali hiyo imetokea katika, barabara ya Same - Mwanga, Kijiji cha Kiverenge wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro ambapo taarifa za awali zinasema  kuwa chanzo chake ni kupasuka kwa tairi ya mbele.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Robert amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema katika ajali hiyo alifariki Abiria mmoja aliyemtaja kwa jina la Joshua Likumbia, Raia wa Kenya, ambaye alikuwa akisafiri kuelekea jijini Mbeya.

Kamanda Boaz amesema majeruhi katika ajali hiyo ambao ni 16, akiwemo dereva wa Basi, Fadhili Hashim wamelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Same na Hospitali ya Rufaa mkoani Kilimanjaro, KCMC.

Kamanda Boaz ameendelea kufafanua kuwa majeruhi hao nane wamelazwa Same huku wengine 8 wakikimbizwa mjini Moshi katika hospitali ya KCMC kutokana na hali zao kuwa mbaya ambapo watatu kati yao wakia wamelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog