Thursday, December 19, 2013

Saida Karoli 

MSANII wa muziki wa asili aliyewahi kutamba na wimbo wa ‘Maria Salome’ uliokuwa maarufu kwa jina la ‘Chambua Kama Karanga’, Saida Karoli amesema umaarufu aliokuwa nao haukufanana na kile alichokitia mfukoni.
Mkali huyo wa Kaisiki na Mapenzi kizunguzungu alisema alitembea nchi nyingi duniani bila kuingiza kipato kikubwa mfukoni mwake kutokana na kulipwa mshahara na meneja wake hata kama angefanya kazi kubwa na shoo zilizoingiza kipato kikubwa.
“Siwezi kuweka wazi mshahara niliolipwa ila nakumbuka nilifanya shoo za kulipwa kwa dola na kuzunguka nchi mbalimbali duniani ila nililipwa kwa fedha ya Kitanzania tena mshahara uleule kila mwezi, nashukuru kwa sasa ninajisimamia mwenyewe ninapata fedha nyingi sana ingawa sina jina kama zamani,” aliweka wazi Saida Karoli.
Kwa sasa msanii huyu ameweka makazi yake jijini Mwanza huku akitamba na wimbo wa Mashamsham na albamu yake ya Pesa Inawasha.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog