Kikosi
cha Young Africans kimewasili jana mjini Kahama ambapo kitaweka kambi
ya siku ya tatu kabla ya kuelekea mjini Bukoba kwa ajili ya mchezo wake
wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara siku ya jumamosi dhidi ya wenyeji
timu ya Kagera Sugar.Young Africans ikiwa mjini Kahama itacheza mchezo wa kirafiki siku ya jumatano dhidi ya wenyeji timu ya Ambassador FC ikiwa ni sehem ya maandalizi ya kocha kuelekea mchezo wa wakata miwa wa mkoa Kagera.
Kocha Marcio Maximo leo asubuhi amekiongoza kikosi chake kufanya mazoezi katika Uwanja wa Taifa mjini hapa ikiwa ni maandalizi ya mechi ya mwishoni mwa wiki dhidi ya Kagera Sugar baada ya kupata pointi tatu katika mchezo dhidi ya Stand United.
RSS Feed
Twitter
12:18 AM
Unknown